Thursday 31 October 2013

UMAGHARIBI NA SANAA JADIA ZA KIAFRIKA



ATHARI ZA KIMAGHARIBI KATIKA SANAA ZA MAONYESHO ZA KIAFRIKA NA FASIHI KWA UJUMLA
Dhana ya fasihi simulizi imekuwa ikijadiliwa kwa miongo mingi na wataalamu mbalimbali kama ifuatavyo:-
Mulokozi, anafafanua kwamba, Fasihi simulizi ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi. Hapa anamaanisha fasihi simulizi ni tukio ambalo hufungamana na muktadha fulani ya kijamii wenye kutawaliwa na fanani hadhira, fani inayotendwa, tukio, mahali na wakati.
Wamitila, (2003) anasema kuwa, fasihi simulizi ni sanaa ya lugha inayotungwa na kubuniwa kwa mdomo bila kutumia maandishi. Aidha fasihi simulizi ni tukio linalofungamana na muktadha fulani wa kijamii na mwingiliano wa fanani, hadhira, fani inayotendwa, tukio, mahali na wakati.

Wednesday 30 October 2013

MAJIGAMBO



SANAA YA MAJIGAMBO KATIKA NYIMBO ZA KIZAZI KIPYA

(UWASILISHAJI)


Kwa hakika sanaa ya majigambo yaijapotea Barani Afrika, isipokuwa imebadilika tu kulingana na maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.
Katika kujadili mada hii, kwanza tutaanza kufafanua dhana ya majigambo kwa kuwatumia wataalamu mbalimbali huku tukitoa maana yetu kutokana na mawazo ya wataalamu hao, pia tutaelezea kwa ufupi kuhusu chimbuko la muziki wa kizazi kipya, kisha tutaingia katika kiini cha mada tajwa kwa kuonesha jinsi gani majigambo yalivyojitokeza katika nyimbo mbili za kizazi kipya ambapo tumetumia wimbo wa msanii Prof Jay “Ndiyo mzee” na wimbo wa Sugu “Sugu”. Kisha hitimisho

Monday 28 October 2013

MAKUTANO YA FASIHI


FASIHI SIMULIZI NA FASIHI MAMBOLEO YA KIAFRIKA

UTANGULIZI:
Maswali ya Udadisi
  1. Fasihi Simulizi ni nini?
  2. Fasihi Mamboleo ni Fasihi ya namna gani?
  3. FS na FM zinahusianaje? (ni tofauti?, ni sawa?,….) Je upo mpaka bayana baina ya FS na FM?
FM……..Fasihi andishi. Huitwa FM kwa sababu kiumri FS ni kongwe zaidi ya FA. Hujumuisha sanaa mbalimbali ziliwasilishwa kwa njia ya maandishi, kama vile riwaya, ushairi, tamthilliya na hadithi fupi. Mijadala mingi ya wanazuoni wa mwanzo kuhusu FS na FA….ilichunguza sana tofauti kati ya sanaa moja na sanaa nyingine. Katika hatua hiyo ya uchunguzi, walidiriki kunena kuwa FA ni fasihi imara na thabiti zaidi ya FS, kwa upande mwingine, wapo walioeleza kuwa FS ni kongwe zaidi ya FA. Katika mjadala wetu, hatutajihusishi sana na majadiliano ya utofauti wa sanaa hizi mbili, bali tunachochunguza ni MWINGILIANO ULIOPO BAINA YA FS NA FA.

Sunday 27 October 2013

SEMANTIKI



SINONIMIA

(UWASILISHAJI)
Neno sinonimia limeelezwa na wataalamu mbalimbali na kwa namna tofauti kama ifuatavyo;
Habwe na Karanje (2004:209), sinonimia ni uhusiano wa kileksia ambapo huwa kuna maumbo katika lugha ambayo maana zake ni sawa. Maumbo haya yanaitwa sinonimu. Basi sinonimu ni visawe vya sinonimia moja.
Yule (1985:95), sinonimia ni maneno mawili au zaidi yenye maumbo yanayohusiana ambayo huweza kubadilishana nafasi katika mazingira fulani lakini sio mazingira yote katika sentensi.
Linsky (1952), sinonimia ni ile hali ya maneno mawili ya lugha kufanana endapo yatakuwa na maana zinazofanana.

Thursday 24 October 2013

KAMUSI



DONDOO KATIKA KAMUSI (CITATION FORMS)

Kulingana na Newell (1995) amebainisha nduni zifuatazo za Kongoo
a.       Maumbo yasiyo na mnyambuo ambayo hutokea katika hali ya Kifonolojia (Matamshi) ndiyo huingizwa katika kamusi mfano; mama, shangazi, sana, suri n.k
b.    Maneno ambayo hayana  viambishi ndiyo hudondolewa katika kamusi mfano; adhimisha, piga, adhimu vinaweza kuwa kidahizo.
c.       Maumbo huru yenye sifa za kifofonemiki huweza kuorodheshwa kama kidahizo. Umbo lenye mkazo mmoja tu.
d.      Maumbo yanayotambuliwa na wazungumzaji asilia wa lugha hiyo kama neno, yanaweza pia kuingizwa katika kamusi kama kidahizo. Hapa ni muhimu kupata tajiriba kutoka kutoka kwa wazawa.
e. Maumbo ambayo ni rahisi kuyabainisha kama neno yanapokuwa katika sentensi, huingizwa katika kamusi kama kidahizo: Kijana mdogo sana amesafiri leo asubuhi kwa ndege ya fastjet
f.      Maumbo yanayotokea mara kwa mara mfano mtoto Vs Kitoto hutumika mara kwa mara katika maandishi na mazungumzo. Katika kongoo ya Kiswahili kuna maneno yapatayo milioni kumi (10,000,000/=).
g. Maumbo yote yale yanayowakilisha maana ya msingi (Basic meaning) ya leksimu huingizwa katika kamusi kama kidahizo mf. Askarikanzu, mpigambizi, amevaa miwani n.k
h. Maumbo ya mashina ambayo maneno nyambulishi mengine yanaweza kuundwa, yanaweza kuorodheshwa pia kama kidahizo
i.       Maumbo yanayoweza kutumika kupata vitomeo vidogo (sub-entry) yanaweza kuingizwa katika kamusi kama kidahizo.

KUSIGANA NA KULANDANA KWA MSAMIATI


KUFANANA NA KUTOFAUTIANA KWA LEKSIKOGRAFIA, LEKSIKOLOJIA NA LEKSIKONI.
Katika kujadili mada hii tutaanza kufasili maana ya leksikografia, leksikolojia na leksikoni kisha tutajadili zaidi kuhusu tofauti zilizopo baina ya leksikografia, leksikolojia na leksikoni na mwishowe tutaweka hitimisho la mada yetu pamoja na marejeo.
Wataalamu mbalimbali wametoa fasili ya Leksikografia kama vile  Mdee (1985) anaeleza leksikografia ni usawiri wa kamusi, Huu ni utaalamu au utaratibu wa kukusanya msamiati pamoja na tafsiri yake na kuupanga katika kitabu cha maneno ambacho huitwa Kamusi.
Fasili hii ya Mdee ina udhaifu kwani Kamusi siyo lazima iwe imeandikwa katika kitabu pekee, bali kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia siku hizi kamusi zimeweza kuandikwa katika elektroniki mfano kompyuta na simu za mkononi.

MAWANDA YA KISWAHILI



MAWANDA YA KISWAHILI KATIKA DUNIA YA UTANDAWAZI.
Utandawazi ulianza polepole kuingia katika lugha ya Kiswahili tangu enzi za utawala wa Kikoloni. Hali hii ilisababisha mabadiliko kadha wa kadha hususani katika lugha ya Kiswahili. Mabadiliko hayo yanaweza kujidhihirisha katika nyanja mbalimblai kama vile; Utamaduni (Dini, na Elimu), Biashara na Utawala. Vyote hivi kwa pamoja vilisaidia kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili ndani na nje ya Afrika.
Utawala wa Kikoloni katika kipindi hicho uliambatana na kuanzishwa rasmi kwa vyombo vya habari kama vile magazeti na redio. Maendeleo yalizidi kuongezeka zaidi na zaidi hasa katika kipindi cha Ukoloni mamboleo, ambapo tunaona vyombo vipya vya upashanaji habari kama vile; luninga, tovuti. barua pepe, simu nk.  Hali hii imesaidia kuimarisha utandawazi wa Kiswahili kuwa na mawanda mapana zaidi kimatumizi.

Saturday 5 October 2013

FANI NA MAUDHUI



FANI NA MAUDHUI KATIKA FASIHI
FANI: huu ni ufundi wa kisanaa autumiao msanii katika kutoa ujumbe wake kwa hadhira iliyokusudiwa. Katika fani kumegawanyika vipengele mbalimbali kama vile wahusika, mitindo, muundo, mandhari, matumizi ya lugha, kufaulu na kutokufaulu kifani. Vipengele muhimu vinavyoangaliwa ni hivi vifuatavyo:
Mtindo; hii ni mbinu ya kipekee kifani na kimaudhui, zinazotofautisha msanii mmoja na mwingine. Kwa mfano, katika riwaya ya “Barua Ndefu kama hii” iliyoandikwa na Mariama Ba ametumia mtindo wa kirafiki kuanzia mwanzo hadi mwisho. Kwa mfano, barua ya Ramatulayi kwa Dauda Dieng na barua kwa Aisatu.

Friday 4 October 2013

TAATHIRA KATIKA FASIHI



MSINGI WA KUWEPO MOTIFU ZA AINA MOJA KATIKA TANZU ANUAI ZA FASIHI ZA MATAIFA/MAKABILA TOFAUTITOFAUTI ULIMWENGUNI.
Katika mada hii tutaanza kufafanua juu ya nadharia ya taathira, mwingiliano matini na usambamba kisha tutafafanua juu ya dhana ya motifu kabla ya kuingia moja kwa moja katika kiini cha mada yetu.
Nadharia ya taathira. Hii ni nadharia iliyoasisiwa na shule ya Ufaransa wakati wa kuchunguza fasihi linganishi katika sehemu mbalimbali ulimwenguni. Guyard, M.F na Tieghem wanafafanua nadharia hii kuwa, uchukuaji wa mawazo kutoka katika kazi moja ya fasihi kwenda nyingine inahusishwa pia na uchukuaji au upelekaji wa wazo kutoka katika aina moja ya jamii kwenda nyingine.
Carre. J.M anaamini taathira ni sawa na upokeaji yaani kazi moja inakuwa na vipengele fulani fulani kutoka fasihi nyingine.
Zhirmunwk anaeleza kuwa ni mchakato wa upokezi usio wa bahati mbaya hivyo mtunzi anautumia kwa makusudio na vipengele hivyo ni vya kiutamaduni na kiitikadi.