DONDOO KATIKA
KAMUSI (CITATION FORMS)
Kulingana na Newell (1995)
amebainisha nduni zifuatazo za Kongoo
a. Maumbo
yasiyo na mnyambuo ambayo hutokea katika hali ya Kifonolojia (Matamshi) ndiyo
huingizwa katika kamusi mfano; mama, shangazi, sana, suri n.k
b. Maneno
ambayo hayana viambishi ndiyo
hudondolewa katika kamusi mfano; adhimisha, piga, adhimu vinaweza kuwa
kidahizo.
c. Maumbo
huru yenye sifa za kifofonemiki huweza kuorodheshwa kama kidahizo. Umbo lenye
mkazo mmoja tu.
d. Maumbo
yanayotambuliwa na wazungumzaji asilia wa lugha hiyo kama neno, yanaweza pia
kuingizwa katika kamusi kama kidahizo. Hapa ni muhimu kupata tajiriba kutoka
kutoka kwa wazawa.
e. Maumbo
ambayo ni rahisi kuyabainisha kama neno yanapokuwa katika sentensi, huingizwa
katika kamusi kama kidahizo: Kijana mdogo sana amesafiri leo asubuhi kwa
ndege ya fastjet
f. Maumbo yanayotokea mara
kwa mara mfano mtoto Vs Kitoto hutumika mara kwa mara katika maandishi na
mazungumzo. Katika kongoo ya Kiswahili kuna maneno yapatayo milioni kumi
(10,000,000/=).
g. Maumbo
yote yale yanayowakilisha maana ya msingi (Basic meaning) ya leksimu huingizwa
katika kamusi kama kidahizo mf. Askarikanzu, mpigambizi, amevaa miwani n.k
h. Maumbo
ya mashina ambayo maneno nyambulishi mengine yanaweza kuundwa, yanaweza
kuorodheshwa pia kama kidahizo
i. Maumbo yanayoweza
kutumika kupata vitomeo vidogo (sub-entry) yanaweza kuingizwa katika kamusi
kama kidahizo.